• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Taaifa Zaidi

5.0. HUDUMA: 

Idara inatoa huduma takribani kwa jumla ya wananchi 192,781 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 wa Wilaya ya Urambo.

5.1: Utoaji wa huduma 

Idara inatoa huduma kwa siku 5 za wiki kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi 9:30 mchana kama ifuatavyo:-

Kutoa vibali vya idhini ya kufyatua matofari katika eneo la Mamlaka ya Mji Mdogo Urambo kwa kiindi cha mwezi Machi hadi Oktoba baada ya kufanya ukaguzi wa eneo husika la vichuguu ili kudhibiti uharibifu wa mazingira.

Kugawa miche ya miti kwa wananchi mwezi Desemba hadi Aprili kila mwaka kwa ajili ya kupanda katika maeneo ya makazi, taasisi na mashamba binafsi ya miti ili kuboresha mazingira.

Kutoa ushauri (Extension services) bure juu ya uoteshaji, upandaji na utunzaji wa miti kwa siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi 9:30 mchana.

Kutoa ushauri bure kwa wawekezaji wa miradi mikubwa ya kibiashara juu ya kufanya tathmini ya athari kwa mazingira kabla ya kutekeleza mradi.

Kuhakikisha huduma bora ya uzoaji taka ngumu na maji taka inatolewa kwa wakati kwa wananchi wanaokaa katika eneo la Mamlaka ya Mji Mdogo Urambo.

6.0. MAJUKUMU YA IDARA

Idara inahamasisha wananchi kutunza mazingira kwa kupanda na kutunza miti ya matumizi mbalimbali ya kuni/nishati kivuli, mbao na matunda pamoja na kutunza uoto wa asili kuboresha mazingira ya Wilaya yetu.

Idara inahamasisha na kusimamia usafi na utunzaji wa mazingira katika maeneo ya makazi, vyanzo vya maji, biashara, stendi, taasisi, vizimba vya kukusanyia taka ngumu, mashirika, viwanda, michezo, maegesho, kumbi za starehe na maeneo ya wazi.

Idara inasimamia taratibu za ukusanyaji wa taka ngumu na unyonyaji wa maji machafu kutoka katika makazi  na maeneo ya shughuli za kibiashara na kupeleka katika maeneo ya dampo yaliyotengwa kwa kazi hiyo ili kudhibiti magonjwa ya mlipuko na uchafuzi wa mazingira.

Idara inatoa ushauri kwa Wananchi wanaotaka kuwekeza katika miradi mikubwa ili waweze kuzingatia Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 inayoelekeza kuzingatia taratibu za tathmini ya athari kwa mazingira kabla ya kutekeleza mradi.

7.0: MPANGO MKAKATI WA USAFI WA MAZINGIRA

SIKU ZA KAMPENI YA USAFI WA MAZINGIRA (KILA JUMAMOSI YA MWISHO YA KILA MWEZI NA KILA ALHAMISI YA KILA WIKI)

JUKUMU LA MWANANCHI AFANYE NINI?

  • Kila mtu atumie vifaa alivyonavyo nyumbani kwake kwa shughuli ya usafi.
  • Kusanya taka na weka kwenye mfuko au dust bin kisha weka eneo ambalo gari / mkokoteni hufika kubeba taka na kupeleka Dampo.
  • Hakikisha eneo la nyumba/biashara yako liko safi (Weka taka katika chombo/dustbin).
  • Kiongozi Msimamizi (M/Kiti wa Kitongoji, M/Kiti wa Soko) atakagua kitongoji chake au soko lake na wataalam wa Afya pamoja na Wasimamizi ngazi ya Wilaya kila Jumamosi ya mwisho ya kila Mwezi.
  • Taarifa ya Utekelezaji wa zoezi itawasilishwa kwa Mkuu wa Wilaya kila Mwezi.

MAJUKUMU YA MJI MDOGO URAMBO IDARA YA USAFI NA MAZINGIRA

Idara hii itashughulika na Ukusanyaji, uzoaji na utupaji wa taka ngumu.

Taka zilizopo katika mifuko/dust bin kwenye vitongoji au mitaa.
Taka toka katika masoko
Taka za stend ya mabasi
Kuondosha Mizoga mbalimbali katika makazi ya wananchi
Taka zilizopo maeneo ya wazi


Mpango kazi (Usafi wa Mji) kwa kutumia vikundi vya kijamii siku ya Jumatatu – Jumamosi.

Saa 1:30 Asubuhi – 2:00 Asubuhi – Vikundi kuandaa na kuchukua vifaa vituoni (Makwama / Guta/ Roli).

Saa 2:00 Asubuhi – 9:30 Mchana – Makwama / Maguta/Magari kupita katika vituo vya kuzolea taka na mizunguko katika vitongoji na kueleka taka dampo. 

8.0. SHUGHULI MBALIMBALI ZILIZOTEKELEZWA NA IDARA

8.1. Utekelezaji wa zoezi la Upandaji Miti katika Wilaya ya Urambo

Serikali, kwa lengo la kuhakikisha kuwa mazingira ya nchi yetu yanarejeshwa katika hali ya ubora, ilitoa agizo kuwa kila Halmashauri ya Wilaya ihakikishe inazalisha na kupanda miche ya miti 1,500,000 kila mwaka.

Jedwali Na. 1: Utekelezaji wa malengo ya upandaji miti kuanzia mwaka 2010/2011 hadi 2017/2018 Wilayani Urambo.

Mwaka

Lengo la upandaji

Miti iliyopandwa

Miti iliyostawi

Ustawi (%)

2010/2011

1,500,000

2,094,235

1,465,965

70

2011/2012

2,000,000

3,500,000

2,555,000

73

2012/2013

2,000,000

3,350,294

2,680,236

80

2013/2014

2,000,000

1,525,663

1,144,248

75

2014/2015

2,000,000

2,647,510

2,065,058

78

2015/2016

1,500,000

1,531,960

1,087,691

71

2016/2017

1,500,000

2,210,119

1,502,880

68

2017/2018

1,500,000

2,684,509

-

-

Jumla

14,000,000

19,544,290

12,501,078

64


HABARI PICHA SOMA HAPA


Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.