• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Historia


UTANGULIZI

Wilaya ya Urambo ni kati ya Wilaya Nane (8) zinazounda Mkoa wa Tabora. Wilaya hii ilianzishwa tarehe 19/07/1975 kwa namba za utambuzi  GN of 185 of 1980  baada ya kugawanywa Halmashauri ya wilaya ya Tabora vijijini na Urambo; wilaya ya Urambo ina Tarafa mbili za Urambo na Usoke,   Kata 18, Vijiji 59  na Vitongoji 254. Mwaka 2013, Halamshauri ya wilaya ya Urambo iligawanya pia katika Hamashauri mbili yaani Urambo na Kaliua.

Mipaka ya Halamshauri ya Wilaya ya Urambo

Wilaya hii imepakana na Wilaya ya Sikonge na Uyui kwa upande wa Mashariki, na inapakana na Wilaya ya Mpanda (Mkoa wa Katavi) kwa upande wa Kusini, kwa upande wa Kaskazini Magharibi inapakana na Wilaya ya Kaliua.

Ukubwa wa Eneo
Halamshauri ya wilaya ya Urambo ina ukubwa wa eneo lenye kilometa za mraba Elfu sita miamoja kumi na moja ( km2 6,110) sawa na asilimia nane (8%) ya eneo la Mkoa wa Tabora. Makao makuu ya Wilaya yapo katika mji mdogo wa Urambo umbali wa kilometa takribani tisini (90 ) kutoka Tabora Mjini


IDADI YA WATU

Kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Wilaya ya Urambo ina jumla ya wakazi wapato 192,781, (Nyamwezi ,Sukuma,Waha,Wafipa,Wasumbwa na wengineo) kati yao Wanaume 95,997 sawa na 49.80% na Wanawake 96,784 sawa na 50.2% . Wilaya ina jumla ya kaya 32,675 kwa wastani wa ukubwa wa kaya moja ni watu 5.9 ongezeko la watu kwa mwaka inakisiwa kuwa 4.8%. 


VIONGOZI WETU

a) b)


HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA WILAYA.

Uchumi wa Wilaya unategemea zaidi kilimo ambacho kinaajiri takribani asilimia 80 ya wakazi wote wa Wilaya hii. Mapato yanayotokana na ufugaji, Uvuvi, Ufugaji wa nyuki na shughuli za viwanda vidogo vidogo ni ajira mbadala zinazochangia katika pato la wakazi wetu.

Pato la Wilaya ya Urambo katika mwaka 2012/2013 hadi Desemba, 2012 lilikuwa Tshs. 77,822,778,064/= ikilinganishwa na idadi ya watu 192,781 na hivyo pato la mtu ni sawa na Tshs. 403,685/=. Aidha wastani wa pato la mtu kwa mwaka liliongezeka kutoka Tshs. 172,000/=mwaka 2002 hadi Tshs. 403,685/= mwaka 2012, sawa na ongezeko la Tshs. 231,685/=.

Hali ya Hewa

Hali ya hewa ya Halmashauri ya wilaya ya Urambo ni ya Kitropiko inatawaliwa na vipindi  vikuu viwili kama ifuatavyo:-


Hali ya Joto ni kati ya 15˚C na 22˚C, joto uongezeka Mwezi wa Tisa, na hali ya 


HALI YA ULINZI NA USALAMA 

Hali ya ulinzi na usalama katika Wilaya yetu kwa ujumla ni nzuri; na hii inachangiwa na uwepo wa ulinzi shirikishi kupitia Polisi jamii. Mpango huu muhimu ni wa kudumu kwa kushirikisha jeshi la mgambo katika suala la ulinzi kwa kuwatambua, kuwajali na kuwathamini.

Hata hivyo wilaya inaendelea kukabiliana na matukio mara kwa mara ya makosa ya jinai yakiwemo ya unyang’anyi wa kutumia silaha na nguvu, Uvunjaji, Wizi wa pikipiki,Wizi wa mifugo,kuchoma nyumba moto n.k. Mauaji yanayotokea katika Wilaya hii mara nyingi yanatokana na kulipiza kisasi, imani za kishirikina na matukio machache ya kugombea mali.

Kufuatia hali hiyo wilaya inashirikiana na Wilaya jirani katika mkakati wa kuimarisha Ulinzi na usalama na kubadilishana taarifa za kiuharifu miongoni mwetu na Wilaya zinazotuzunguka. 

HALI YA UTOAJI HUDUMA KISEKTA

Shughuli ambazo zimekuwa zikitekelezwa na Wilaya kisekta katika utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kama ifuatavyo:-

SEKTA YA UTAWALA NA UTUMISHI.

Wilaya ina jumla ya watumishi 1,458 kutoka katika kada mbalimbali za utumishi kama zifuatavyo:- Utawala na Utumishi 100, Elimu Sekondari 209,Elimu Msingi 835 , Afya 215, Kilimo Umwagiliaji na Ushirika 15,Mifugo na Uvuvi 9,Ardhi na Maliasili 6, Maji 7, Ujenzi 18, Watendaji wa Vijiji 43 na Usafi na Mazingira 1.

CHANGAMOTO

Watumishi walioajiriwa kuomba kuhama kufuata wenzi wao baada ya kukaa muda

Ufinyu wa bajeti

Utoro kazini

Watumishi wapya Kushindwa kuripoti na Serikali kutoleta watumishi kulingana na ikama iliyoidhinishwa.

gana na ikama iliyoidhinishwa.


Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.