• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Baraza la Madiwani lapongeza usimamizi bora wa shughuli za Halmashauri

Siku iliyowekwa: September 12th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Urambo limekutana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo tarehe 12.09.2024 kwa ajili ya kufanya mkutano wa mwaka, ambapo mkutano huo umepokea taarifa ya shughuli mbalimbali zilizotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Urambo katika kipindi cha mwezi Julai 2023 hadi Juni 2024.


Mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Adam Malunkwi, umepokea taarifa hiyo kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ambapo taarifa hiyo imegusa mapato na matumizi pamoja na mafanikio, changamoto na mikakati ya Halmashauri katika kutekeleza shughuli mbalimbali katika mwaka mpya wa fedha 2024/2025.


Akiwasilisha taarifa hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ililenga kukusanya kiasi cha Tsh. 3,076,270,000 kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani. Hata hivyo hadi kufikia Juni 30, 2024 Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ilifanikiwa kukusanya kiasi cha Tsh. 3,510,090,017.09 ambayo ni sawa na asilimia 114 (114%) hivyo kuvuka lengo la makusanyo katika Mwaka wa fedha 2023/2024.


Aidha Mkurugenzi Quintine amesema pamoja na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Halmashauri katika mwaka wa fedha 2023/2024, Halmashauri ilipata mafanikio mbalimbali kupitia divisheni, idara pamoja na vitengo vyake ambapo ni pamoja na kufanikisha ujenzi na ukamilishaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, uboreshaji wa huduma mbalimbali n.k


Baada ya kuwasilishwa kwa taarifa hiyo wajumbe waliweza kupongeza kwa taarifa nzuri pamoja na kupongeza usimamizi bora wa shughuli za Halmashauri hasa katika ukusanyaji wa mapato kwani ni mara ya kwanza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato ya ndani. hata hivyo wajumbe waliweza kupongeza mafanikio mengineyo ambayo Wilaya iliyafikia katika mwaka wa fedha 2023/2024 ikiwemo kushika nafasi ya kwanza Kitaifa katika Mbio za Mwenge wa uhuru wa Mwaka 2023.

Aidha, pamoja na kupokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Halmashauri, Mkutano huu ulifanya uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti pamoja na Wenyeviti wa kamati mbalimbali za Halmashauri ulioenda sambamba na uteuzi wa wajumbe wa kamati hizo kulingana na sheria na kanuni.


"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, jitokeze kushiriki Uchaguzi"

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.