• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Muinueni Mtoto Wa Kike Wa Urambo Kupenda Masomo Ya Sayansi

Siku iliyowekwa: December 10th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine amesema kinachopelekea Watoto wa Kike kutopenda kusoma masomo ya Sayansi ni kutokana na kukatishwa tamaa na watu wanaowazunguka. 

Bi. Quintine amesema hayo wakati akifungua Semina ya siku mbili ya kuhamasisha Mtoto wa kike kupenda na kusoma masomo ya Sayansi Wilayani Urambo.


Kampeni hiyo inayohusisha Semina pamoja na ufuatiliaji wa matokeo inayofadhiliwa na Shirika la UNICEF imefanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Kitaifa ya Wasichana ya Margareth Sitta na kuhusisha Walimu Wakuu wa shule za Sekondari 17, Walimu wa masomo ya Sayansi, Viongozi wa Serikali za Vijiji na Vitongoji pamoja, Viongozi wa dini pamoja na wawakilishi wa wazazi.


Katika ufunguzi wa Semina hiyo Mkurugenzi Quintine amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amejikita katika kuweka usawa wa kijinsia katika nyanja mbalimbali, lakini pasipo na watoto wa kike wengi wenye elimu itakuwa ngumu kupata wanawake wa kufaa katika nafasi hizo. Hivyo amesisitiza kuwa Washiriki wa semina hiyo kuwa makini katika mafunzo watakayopewa ili wawe mabalozi wazuri wa kuhamasisha wazazi na watoto wa kike kusoma masomo ya Sayansi.


Aidha Bi. Grace Quintine amesema kuwa Mtoto wa Kike ana upeo mkubwa wa kiakili ambapo anaweza kusoma masomo hayo na kufaulu vyema kwani hata yeye alifaulu masomo hayo kwa kuyasoma kwa miezi kadhaa alipokuwa Sekondari, Hivyo amewaasa wawaelimishe wazazi kuepuka mawazo potofu ya kuwa mtoto wa kike hana manufaa kwa mzazi kwani mtoto wa kike ni rahisi zaidi kumhudumia mzazi wake pale anapopata uwezo wa kufanya hivyo.


Hata hivyo amesema jamii inapaswa kuepukana na Mila kandamizi kwa Mtoto wa kike kwani watoto wote wa kike na wakiume wana haki sawa.


Amehitimisha kwa kusema kuwa kumkatisha tamaa na kumuozesha mapema mtoto wa kike kabla hajatimiza ndoto zake ni kuharibu viongozi wa kesho watakaohudumia jamii, hivyo jamii inapaswa kuwapa moyo watoto wa kike kila mtu kwa nafasi yake ili kupata viongozi bora wajao.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.