• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Urambo yapokea Bilioni 3.6 za Miradi Mipya ya Elimu

Siku iliyowekwa: July 16th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Urambo imepokea fedha kwa ajili ya Utekelezaji wa Miradi 10 ya Elimu, fedha jumla ya Shilingi Bilioni 3.6

Miradi hii imeweza kutambulishwa katika kikao kazi kilichofanyika Tarehe 16 Julai, 2024 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo na Kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt. Khamis A. Mkanachi (Mgeni Rasmi), Katibu Tawala wa Wilaya ya Urambo Ndg. Innocent Nsena, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mhe. Adam Malunkwi, Afisa Usalama (W), Kamanda wa TAKUKURU (W), Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ndg. Shabani Mussa, Katibu wa CCM Wilaya Ndg Himis Tweve, Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margareth Sitta, Wahe. Madiwani wa Kata husika zenye Miradi, Wakuu wa Divisheni na Vitengo, Watendaji Kata na Maafisa Elimu Kata, Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji, Watendaji  wa Vijiji, Waratibu wa Miradi pamoja na Maafisa Masuuli Wateule (Wakuu wa Shule)

Akizungumza Katika kikao kazi cha kutambulisha Miradi hiyo, Mhe Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt. Khamis A. Mkanachi amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine kwa uwazi wake wa kushirikisha wadau mbalimbali kufahamu, kuandaa na utekelezaji wa Miradi hiyo, hatua ambayo itachangia ukamiliishwaji wa Miradi hiyo kwa wakati na kama ilivyokusudiwa.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa pongezi hizo. Aidha Bi. Quintine ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha hizo kwa ajili ya Utekelezaji wa Miradi hiyo ambayo inaenda kuinua Sekta ya Elimu Wilayani Urambo.

Sambamba na Hilo amemshukuru na Kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margareth Sitta kwa juhudi zake za dhati pamoja na ushirikiano wake na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji pamoja na jitihada za kufuatilia na kuhakikisha fedha za miradi hiyo zimepatikana.

Sambamba na Hilo Bi. Quintine amesisitiza Ukamilishaji wa Miradi ndani ya muda uliopangwa, kufuata utaratibu wa usimamizi wa Utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na Ushirikiano baina ya Maafisa Masuuli wateule na Afisa Masuuli Mkuu (Mkurugenzi Mtendaji). Sambamba na Hilo Bi Quintine ametilia mkazo hoja ya Mhe. Dkt. Khamis A. Mkanachi ya kuweka mpango kamili kabla ya kuanza utekelezaji wa Miradi (Kujengea Mezani).

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt. Mkanachi amesisitiza ushirikishwaji wa wananchi katika Miradi hiyo na kutumia wananchi kwa 20% kwa ajili ya nguvu kazi kwenye utekelezaji wa Miradi.

Miradi hiyo itatekelezwa katika Kata Nane za Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ambapo kutakuwa na ujenzi wa mabweni na Shule mpya za Msingi na Sekondari zitakazojengwa mwaka huu.

Umaliziaji wa Bweni Shule ya Sekondari Urambo Day Kata ya Kiyungi gharama ya Mradi ni TSh. 136,123,769.92/= (EP4R)

Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi Katika Kata ya Kiyungi Gharama ya Mradi ni Tsh. 364,500,000/= (BOOST)

Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Muungano gharama ya Mradi Tsh. 603,890,563.000/= (SEQUIP)

Ujenzi wa Mabweni Mawili katika Shule ya Sekondari Usoji Kata ya Songambele Gharama ya Mradi Tsh. 272,000,000/= (EP4R)

Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Shule ya Sekondari Igunguli kata ya Uyogo Gharama ya Mradi ni Tsh. 110,000,000/= (SEQUIP)

Upanuzi wa Shule ya Sekondari Kasisi kuwa ya Kidato cha Tano na Sita (A-Level) Kata ya Kasisi gharama ya Mradi ni Tsh. 398,000,000/= (SEQUIP)

Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Kata ya Nsenda gharama ya Mradi ni Tsh. 603,890,563/= (SEQUIP)

Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi katika Kijiji cha Kamalendi Kata ya Ukondamoyo Gharama ya Mradi ni Tsh. 364,500,000/= (BOOST)

Upanuzi wa miundombinu ya Kidato cha 5 na 6 katika Shule ya Sekondari Uyumbu Kata ya Uyumbu Gharama ya Mradi ni Tsh. 398,000,000/= (SEQUIP)

Ujenzi wa Vyumba vitatu vya Madarasa, Mabweni 2, na vyoo Matundu 6 Katika Shule ya Sekondari Uyumbu kwa Ufadhili wa Barrick Gharama ya Mradi ni Tsh. 363,200,000/= (BARRICK)

Jumla ya Fedha zote zilizotolewa kwa ajili ya Miradi Mipya itakayoanza kutekelezwa mwaka huu ni Tsh. 3.614,194,895.92.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.