• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

WANAWAKE ITUMIENI IDADI YENU KULETA MABADILIKO

Siku iliyowekwa: March 4th, 2025

"Ombi langu kwenu umuhimu wa wakinamama usibaki katika idadi  kwa maana ya namba, hii idadi mkaigeuze ikalete matokeo na mabadiliko ambayo tunayoyataka" 

Maneno haya yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Dkt Khamis Mkanachi ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Kongano la Wanawake la kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake ngazi ya Wilaya.


Kongamano hilo limefanyika leo tarehe 04.03.2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ikiwa ni kuelekea katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake Ngazi ya Mkoa na Taifa tarehe 08.03.2025.

Katika Kongamano hilo lililogusa mada mbalimbali kama Afya ya Akili, Elimu ya Fedha na uchumi, Elimu kuhusu Saratani ya shingo ya kizazi/mji wa Uzazi, Lishe n.k wanawake na Wasichana wa Urambo walioshiriki waliweza kufaidika na mada hizo.


Aidha Mhe. Dkt. Mkanachi amewaeleza Wanawake kuwa katika maisha ya kila siku Wanawake na Wanaume wanategemeana na maumbile siyo udhaifu kwa namna yoyote ile.


Ikumbukwe kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mara ya kwanza imeongozwa na Rais Bingwa na Kinara Mwanamke ambaye ni Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anayeiongoza vyema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Serikali ya Awamu ya Sita


Aidha  Jimbo la Urambo linawakilishwa na Mwanamke katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mhe. Margaret Sitta anayetetea na kuwasilisha hoja na changamoto mbalimbali kwa niaba ya Wananchi wa Urambo.

Sambamba na hilo, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo inaye Mkurugenzi Mtendaji Kinara Mwanamke, anayeisimamia vyema na kuhakikisha Miradi na shughuli nyingine nyingi za Serikali zinatekelezwa katika kiwango cha Kuridhisha. Naye si Mwingine ni Bi. Grace Quintine.


Aidha katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024, Urambo imepata Wenyeviti wa Vijiji pamoja na Vitongoji wanawake watakaoongoza na kusaidia jamii ya Wananchi wa Urambo. Hivyo basi, Urambo tunatambua, tunaheshimu na kuona kwa Macho mchango wa Mwanamke katika jamii kutoka Ngazi ya Taifa, Jimbo, Halmashauri ya Wilaya pamoja na Serikali za Vijiji na Vitongoji.


Aidha mapema hii leo Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margareth Sitta ameongoza umati wa Wanawake wa Urambo katika Matembezi maalumu ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake ngazi ya Wilaya.

Matembezi hayo yamehusisha Wanawake kutoka Makundi mbalimbali Wilayani Urambo wakiwemo Viongozi wa Dini, Siasa, Vyama vya Wafanyakazi, wajasiriamali, Watumishi wa Umma kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Urambo n.k
Aidha umati huu wa Wanawake umefanya Matembezi kwa lengo la Kuelimisha na Kuikumbusha jamii juu ya umuhimu wa Mwanamke katika Jamii na umuhimu wa kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake kama Siku maalumu ya kutambua mchango wa Mwanamke katika Jamii.

"Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji"

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • URAMBO YAFANIKISHA KIKAO CHAKE CHA KWANZA KUPITIA E-BOARD

    April 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.