• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Wapendeni na Kuwajali Walimu: DC Urambo

Siku iliyowekwa: September 27th, 2022

Mhe. Louis P. Bura Mkuu wa wilaya ya Urambo ameitaka jamii ya Urambo kuwathamini, kuwapenda na kuwajali walimu kwa kiwango cha juu sana kwa sababu walimu ndiyo  wana muda mwingi wa kukaa na watoto wao na hivyo  nafasi kubwa ya malezi ya watoto wanayo walimu, na kuwajali walimu itawaongezea morali ya ufundishaji  na watoto watafanya vizuri kupitia mitihani ya ndani na ya Kitaifa hivyo kuongeza ufaulu wa wilaya.

Mhe. Bura amaeyasema hayo hii leo Septemba 27, 2022 kupitia hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa  Elimu na Mikakati yake ngazi ya wilaya katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Urambo. 

Mhe. Bura amewataka  Wadau wa Maendeleo ya ELimu Urambo wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo,  Watendaji  wa Kata, Waratibu Elimu Kata , Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu kuutumia Mwongozo huu kuhakikisha malengo ya Taifa hasa mikakati iliyobainishwa inafikiwa kwa kutatua changamoto za elimu katika eneo lao bila kungojea viongozi  wengine  kwa lengo la kuhakikisha ufundishaji bora unafikiwa.

Mhe. Bura amewasihi Wadau wa Maendeleo ya Elimu Urambo kuacha kukata tamaa hasa wanapokutana na changamoto, "ni marukufuku kukata tamaa unapokutana na changamoto, kiongozi bora ni yule anaetatua changamoto na sisi tutafanya hiyo kazi kama tulivyokuwa tunafaya siku zote kwa ajili ya watu wa urambo, nasema siku zote wekeni mahusiano mazuri na jamii mkitaka kupunguza upungufu wa miundombinu katika shuke zetu " amesema Mhe. Bura.

Aidha,  Mhe. Bura amewataka Wadau wa maendeleo ya Elimu Urambo kurejesha hali ya utendaji kazi kwa walimu kwa kuwasikiliza vizuri walimu na kubeba matatizo yao yote pindi wanapowasikiliza na kuwataka kutoa mrejesho wenye tija na kwa wakati. Kufanya hivyo kutawafanya walimu kutulia na kufundisha madarasani kuliko kutumia muda mwingi kuja Halmashauri kwa jambo ambalo lingetatuliwa huko huko kituoni.

Mhe. Bura amehitimisha kwa kuwaomba Wadau wa Maendeleo ya Elimu Urambo hasa Maafisa Elimu Kata kusimamia Mwongozo wa Elimu na Mikakati iliyotolewa bila kuupindisha na kuwataka ifikapo Oktoba 1, 2022 Mwongozo huu uwe wazi na bayana kwa walimu wote maana wao ndiyo kiungo cha Afisa Elimu wilaya na walimu wetu.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • URAMBO YAFANIKISHA KIKAO CHAKE CHA KWANZA KUPITIA E-BOARD

    April 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.