• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

Siku iliyowekwa: May 13th, 2025

Urambo, Tabora.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine, leo tarehe 13.05.2025 amekabidhi jezi seti nne kwa Maafisa Elimu  kutoka divisheni za Elimu ya awali na Msingi pamoja na divisheni ya Elimu Sekondari. Jezi hizo zilizoambatana na Mipira miwili, ni vifaa vilivyopatikana kupitia jitihada za dhati za Mkurugenzi Mtendaji aliyeungana na Watumishi wa Kitengo cha Utamaduni Sanaa na Michezo, Maafisa Elimu Sekondari na Msingi kwa kuchangia ununuzi wa vifaa hivyo kwa ajili ya wanafunzi watakaoshiriki UMITASHUMTA na UMISSETA 2025.

Aidha akizungumza katika tukio la utoaji wa vifaa hivyo Bi. Grace Quintine amesema kuwa, UMITASHUMTA na UMISSETA ni matukio makubwa ya Kitaifa hivyo amewasisitiza Maafisa Elimu kuendelea kufanya maandalizi yaliyo bora zaidi ili wanafunzi waweze kushiriki vyema katika michezo hiyo.Ikumbukwe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine, ni mdau mkubwa wa michezo katika ngazi mbalimbali za Kitaifa, ambapo amekuwa akiunga mkono timu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kushiriki katika michezo mbalimbali hapa nchini. Hivyo utoaji wa jezi hizo pamoja na mipira ni muendelezo wa uungwaji mkono wa shughuli za michezo katika nyanja mbalimbali Wilayani hapa.


Katika hatua nyingine, Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Mrgaret Sitta ameungana na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo na kuongeza nguvu katika maandalizi ya UMITASHUMTA na UMISSETA kwa kuchangia fedha taslimu.

Mchango wa Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta kwa ajili ya wanafunzi wanaoshiriki UMITASHUMTA na UMISSETA Wilayani Urambo umewasilishwa na kupokelewa na Mkurugenzi Mtendaji kwa ajili ya kuongeza katika mahitaji ya wanamichezo. Mchango huo umewasilishwa katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji mnamo tarehe 13.05.2025 na Bw. Leonard Malubi - Katibu wa Mbunge kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Urambo. Mhe. Margaret Sitta ametoa fedha taslimu jumla ya Shilingi Milioni mbili (2,000,000) ambazo zitakwenda kusaidia katika maandalizi ya ushiriki wa wanamichezo hao.


Aidha siyo mara ya kwanza kwa Mbunge wa Jimbo la Urambo Mhe. Margaret Sitta kuchangia katika michezo, kwani mara kwa mara amekuwa akichangia na kuandaa mashindano mbalimbali ya kimichezo kwa ajili ya vijana na wananchi wa Urambo. Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo inaunga Mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutia mkazo katika ukuaji wa sekta ya michezo na ukuzaji wa vipaji nchini. Hivyo kwa mwaka huu 2025 Wanafunzi watashiriki mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.


Kazi Iendelee

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.