• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Pro.Ndalichako Akata Utepe VETA-Urambo

Siku iliyowekwa: July 9th, 2019

Waziri wa Elimu Sayansi na Technolojia Pro. Joyce Lazalo Ndalichako(Mb) amezindua Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi cha wilaya ya Urambo (VETA Urambo) katika hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyikia katika viwanja vya Chekeleni kata ya Ussoke Jumanne ya 09.07.2019 wilayani Urambo. Kwa sasa VETA Urambo chenye uwezo wa kudahili wanafunzi 160 kitatoa mafunzo ya ufundi stadi kwa kozi ndefu kwa kipindi cha mwaka 1 katika fani 4 za Ushonaji wa Nguo(Tailoring), Umeme wa Majumbani (Domestic Electrical Installation -DEI), Uashi(Masonry and Bricklaying -MB) na Uhazili na Kompyuta (Secretarial and Computer SC) na mafunzo haya yanaanbatana na masomo ya Hesabu, Engineering Science, Kingereza, Michoro, Ujasiliamali, Stadi za Maisha na Usalama kazini.

Akihutubia umati wa wananchi, viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa  VETA kanda ya Magharibi, Prof.Ndalichako amesema Serikali ya awamu ya Tano imejipanga kuhakikisha kila wilaya nchini inakuwa na Chuo cha Elimu na Mafunzo ili kuwezesha watanazania kupata ujuzi wa fani mbalimbali ili waweze kujiajili na kuajiliwa katika vianda vinavyoendelea kujendwa nchini kwa kadri ya mahitaji ya soko la ajira.

Pia Prof. Ndalichako ameutaka uongozi wa wilaya ya Urambo na viongozi wa VETA Urambo kuhakikisha raslimali yakiwemo Majengo, miundombinu mingine inayotarajiwa kujengwa pamoja na mipaka ya chuo kutunzwa na kulindwa vizuri wakati Serikali ikijiandaa kutuma timu ya wataalamu kuja kufanya tathmini ya ujenzi wa Bwalo la chakula, Karakana ya Ufundi wa Magari(motor vehicle mechanics), Madarasa ya Uungaji wa Vyuma (welding and Fabrication), Ufundi Bomba, Ukarimu wa Holeti (Hotel Management), Ukumbi Mkubwa  na Mabweni ya Wanafunzi.

Awali Mhe. Magreti Simwanza Sitta(Mb) Jimbo la Urambo wakati wa kusalimi wananchi na kutoa shukrani kwa mgeni rasmi prof. Ndalichako, amewasihi wananchi wote wa Urambo kutumia fursa hii ya kipekee ya Chuo cha Ufundi Stadi VETA Urambo kuleta watoto wao hasa wa kike kujifunza fani mbalimbali zitakazotolewa na VETA Urambo. Kwa unyenyekevu Mhe. Sitta amewaomba watendaji wa Vijiji, wenyeviti wa Vijiji vyote 62 vya Urambo kutambua watoto wenye uhitaji wa kujiendeleza katika fani za VETA Urambo na kutoa ahadi ya kugharamia kiasi cha Tsh 60,000/= kwa mwanafunzi mmoja atayesoma VETA Urambo kutoka kila kijiji cha Urambo.

Akitoa ufafanuzi zaidi  Ndg. Eliya Ndiwu mkuu wa chuo cha VETA Urambo ameomba wananchi wa Urambo, mkoa wa Tabora na kote nchini kuleta watoto wao katika chuo hii kwani walimu wabobezi wakutosha wapo, madarasa ya kisasa yenye vifaa vya kujifunza na kufundishia pia vinapatikana chuoni hivi sasa. Ndg. Ndiwu  ameleza sifa za kujiunga kuwa ni elimu ya darasa la saba na kuendelea isipokuwa kwa fani  Uhazili na Kompyuta elimu ni kidato cha 4, na upatikanaji wa fomu ni katika vyuo vyote vya VETA nchini kuanzia tarehe 10.07.2019 hadi 25.07.2019. Pia ametoa mawasiliano ya chuo cha VETA Urambo kuwa ni VETA Urambo Box 1218 Tabora simu +255 787 682 697 na +255 765 765 790 na barua pepe ya vetawesternzone@veta.go.tz

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.