• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Sekondari 14 Urambo Zapata Huduma ya Intaneti

Siku iliyowekwa: October 20th, 2019

Na. Edward Rumanyika, Urambo

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilisano, Mhe. Isack Kamwelwe amezindua huduma ya mtandao wa mawasiliano ya intaneti kwa shule za Sekondari 14 zilizopo Wilaya ya Urambo mkoani Tabora, ili kuwawezesha wanafunzi kupata maarifa kupitia mfumo wa intaneti.

 Mhe. Kamwelwe amezindua huduma hiyo Oktoba 19, 2019 katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Kutwa ya Urambo kufuatia Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania kukubali kutoa huduma hiyo baada ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kutoa kompyuta 70 zenye thamani ya shilingi milioni 140 kwa shule hizo.

Katika kuunga juhudi za UCSAF na kufanikisha huduma za intaneti, Vodacom Tanzania imeongeza kompyuta mpakato (Laptop) 28 na vifaa vya kuwezesha kupata intaneti (routers) 14 vyenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 68 kwa shule hizo ili wanafunzi waweze kujifunza kupitia mfumo wa TEHAMA.

Shule za Sekondari zilizonufaika na msaada huo ni Kapilula, Usisya, Imalamakoye, Chetu, Urambo, Uyumbu, Matwiga, Mukangwa, Kiloleni, Usongelani, Ukondamoyo, Ukombozi, Usoji na Vumilia.

Katika hafla hiyo, Waziri Kamwelwe ameeleza kufurahishwa na msaada ulitolewa na UCSAF na Kampuni ya Vodacom Tanzania na kusema kuwa msaada huo ni chachu ya kuendeleza jitihada za Serikali katika kukuza elimu nchini.

“Kwa niaba ya Serikali napenda kuwapongeza kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukuza elimu, na nitoe rai kwa Afisa Elimu Wilaya na Walimu kwa ujumla kuhakikisha vifaa hivi vinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo”, alisisitiza Mhe. Kamwelwe.

Waziri Kamwelwe alitia ubani katika msaada uliotolewa kwa kuahidi kompyuta 5 kwa kwa kila shule, kwa shule tatu mpya za Sekondari Imala, Uyogo na Ugalla ambazo zimeanzishwa mwaka huu katika Wilaya  ya Urambo ili nazo zisiachwe nyuma katika kutumia huduma za TEHAMA.

 Alieleza kuwa mpango wa awali wa Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha shule za Sekondari 151 za umma zinaunganishwa na huduma ya intaneti kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu.

 Akizungumza kwa niaba ya Serikali na wananchi wa mkoa wa Tabora, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Agrey Mwanri alisema jambo linalotendeka katika shule ya Sekondari ya kutwa ya  Urambo ni kubwa na linagusa mkoa hivyo akashukuru Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote na kampuni Vodacom Tanzania kwa kurudisha sehemu ya faida yao kwa jamii na kuzitaka kampuni nyingine zinazotoa huduma katika mkoa wa Tabora kuiga mfano katika kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Afya na Elimu.

“Sisi hapa mpango tulio nao na tunaoenda nao ni  kwamba kila nyumba ya Mnyamwezi itupatie graduate (mhitimu) wa chuo kikuu  na ili kufikia lengo la kuwa na mhitimu wa chuo kikuu mkoa tunalenga kila mwanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita atembee na kompyuta mpakato mkononi na tutafanikiwa kwa kuunganisha nguvu zetu kama mkoa na kupitia wahisani wa maendeleo kama walivyofanya leo Vodacom Tanzania pamoja na UCSAF”, alieleza Mkuu wa Mkoa.

Awali, akisoma taarifa ya mapokezi ya kompyuta na vifaa wezeshi vya intaneti, Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Angelina Kwingwa, alielezea changamoto zinazozikabili baadhi ya shule, zahanati  na maeneo mengine ya wilaya kuwa ni kokosekana kwa nishati ya umeme na mawasiliano hafifu ya simu za mkononi na kumuomba Waziri kuyataka makampuni ya simu kujenga minara ya mawasiliano ili kungeza ufanisi wa huduma za mawasiliano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Vodacom Foundation, Rosalynn Mworia alieleza kuwa mbali na kutoa kompyuta mpakato na vifaa vya intaneti kampuni hiyo pia inalengo la kutoa mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wawili kutoka kila shule iliyonufaika na vifaa hivyo ili kuwajengea uwezo wa kuvitumia wakati wa kujifunza na kufundisha.

Pia vodacom wametoa tovuti (instant schools.vodacom.co.tz) yenye maudhui ya elimu inayopatikana bure kupitia vodacom kwa lengo la kumsaidia mwalimu na mwanafunzi kupakua vitabu mbalimbali, nukuu za masomo, rejea za mitihani ya miaka ya nyuma ili waweze kujisomea kupitia huduma ya  TEHAMA.

-Mwisho-

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.