• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Urambo yagawa Madawati 819 kukabili upungufu wa Madawati katika Shule zake

Siku iliyowekwa: September 19th, 2024

Wilaya ya Urambo imegawa madawati 819 ikiwa ni awamu a Pili katika shule 13 kwa ajili ya kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati na kuboresha sekta ya elimu.

Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa madawati hayo, Mkurugenzi Mtendaji amesema  kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo inatekeleza dhima ya Serikali kwa kuhakikisha wanafunzi katika shule zote za msingi na sekondari wanakaa kwenye madawati.

Na katika kuhakikisha hilo linatimia, tarehe 19.08.2024 Wilaya ya Urambo imegawa madawati 819 katika shule 13 ili kupunguza uhaba wa madawati katika shule hizo.

Akizungumzia kuhusu kampeni ya kumaliza tatizo la uhaba wa madawati Urambo, Bi. Grace Quintine amesema kuwa Wilaya ya Urambo ilianzisha kampeni ya kutengeneza madawati baada ya kubaini uwepo wa upungufu wa madawati 7,225 kwa shule za msingi na viti na meza 649 kwa shule za sekondari. Hivyo Mhe Mkuu wa Wilaya aliyekuwepo wakati huo SACC. Elibariki Bajuta kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya aliamua kuanzisha kamopeni hiyo kupitia kauli mbiu isemayo "Dawati ni Elimu, Kukaa chini Urambo sasa basi" na kufanikiwa kugawa madawati 1,584 Katika awamu ya Kwanza na awamu hii ya pili madawati 819 na kufanya jumla ya madawati yaliyogawiwa kufikia 2,403.

Madawati hayo 819 yametoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kwa mchanganuo ufuatao JTI madawati 300, Halmashauri ya Wilaya madawati 137, HALEM Construction madawati 14, Gereza la Kilimo madawati 10 pamoja na michango ya wadau mbalimbali yenye jumla ya madawati 358 hivyo kufanya jumla ya madawati yote kuwa 819.

Mkurugenzi Quintine amesema pamoja na kutengeneza asilimia kubwa ya madawati hayo kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri, amewashukuru wadau wa maendeleo waliofanikisha kupatikana kwa madawati mengine mengi katika awamu zote mbili na kusaidia kupunguza tatizo la uhaba wa madawati Urambo.

Hata hivyo Bi. Grace Quintine amesema kwa hatua hii ya mwanzo wameanza na shule zenye uhitaji wa haraka na wataendelea kugawa madawati kadiri yanavyotoka katika Vituo ambavyo vinatengeneza lengo ni kila shule ipate madawati ya kutosha.

Aidha Mkurugenzi Quintine amewahimiza Wanaurambo kuwa watoto wapelekwe shule kwani Serikali imeandaa mazingira mazuri, na wakati huu Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za Msingi mbili (02) na Sekondari mbili (02) Wilayani Urambo  ambapo mpaka Januari 2025 shule zitakuwa tayari ili kuweza kupokea wanafunzi wapya.

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Dkt. Khamis Athumani Mkanachi baada ya kupokea taarifa hiyo amepongeza jitihada za mtangulizi wake SACC. Elibariki Simon Bajuta kwa juhudi zake katika kuanzisha kampeni hiyo ambapo hadi sasa madawati hayo yanaendelea kutengenezwa na kuweza kugawiwa kwenye shule mbalimbali kwa ajili ya kupunguza uhaba wa madawati. Hata hivyo Dkt. Mkanachi amesisitiza kuwa ataendeleza yale yote mazuri yaliyoanzishwa na watangulizi wake ili Urambo izidi kusonga mbele.


"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, jitokeza kushiriki Uchaguzi"

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.