Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine amekutana na Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (Sokoine University of Agriculture - SUA), waliofika Wilayani Urambo kwa ajili ya kufanya utafiti juu ya uendelevu wa misitu kulingana na matumizi ya sasa katika matumizi mbalimbali ya binadamu ikiwemo kilimo cha Tumbaku.
Bi. Grace Quintine amefanya kikao na wataalamu hao katika ofisi yake mnamo tarehe 09.06.2025 na kuzungumza nao juu ya namna ambavyo Kilimo cha Tumbaku kinaathiri misitu, na kuwaeleza juu ya mipango ya Wilaya ya kuhakikisha mazingira yanaendelea kutunzwa na misitu kuendelea kuwepo katika Wilaya ya Urambo.
Aidha amewasihi wafanye utafiti wao katika Wilaya nzima ya Urambo juu ya vyanzo vingine vinavyochangia kuhatarisha uwepo wa misitu kwa matumizi yajayo, na kuwaomba pia kuja na njia na za kunusuru misitu ili ziweze kutumika.
Wataalamu hao kutoka SUA wamekuja kwa mwaliko kutoka katika kampuni ya Tumbalu ya Mkwawa Leaf Tobacco Ltd, kwa lengo la kufanya utafiti unaowagusa wakulima na wadau wa kampuni hiyo ili kuweza kuona kama rasilimali zilizopo zinatosha na zinakidhi mahitaji ya muda mrefu.
Bomani Urambo
Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora
Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824
Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141
Barua pepe: ded@urambodc.go.tz
Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.