• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Mradi wa Umwagiliaji Ussoke Mlimani

Start Date: 2012-07-01
End Date: 2020-06-30


1. UTANGULIZI

Wilaya ya Urambo ina jumla ya hekta 87,984 zinazofaa kwa kilimo, kati ya hizo hekta 10,400 zinafaa kwa kilimo cha Umwagiliaji ,eneo hili ni sawa na 11.8% ya eneo linalofaa kwa kilimo. Wilaya ina skimu moja inayotekeleza kilimo cha umwagiliaji.Kilimo katika Wilaya ya Urambo kinategemea mvua kwa sehemu kubwa.

2. UTEKELEZAJI WA MRADI WA UMWAGILIAJI USSOKE MLIMANI

Mradi  wa Ussoke Mlimani upo katika Tarafa ya Ussoke, kata ya Uyumbu na unatekelezwa na vijiji vya Ussoke Mlimani na Yela Yela. Malengo makuu ya mradi ni kuchangia katika  kuwezesha kufikia lengo la usalama wa chakula (kwa Kaya,na Taifa) kwa kuongeza uzalishaji wa chakula kupitia skimu za umwagiliaji zilizo jengwa au kuendelezwa vizuri. Vile vile kuongeza kipato kwa jamii ili kuwezesha kuondoa au kupunguza umaskini kwenye jamii.

Mradi ulianza kutekelezwa mwaka 2009/2010 kwa kufanya tafiti mbali mbali za upimaji wa sura ya ardhi,usanifu, upimaji udongo na utafiti wa athari za mazingira. Kazi za ujenzi wa bwawa zilianza kutekelezwa msimu wa 2011/2012. Kampuni ya Lead Com and Amp JV ya Box 7240 Dar es salaamu ilitekeleza kazi za ujenzi wa bwawa kwa gharama ya shilingi 326,526,565.00.Bwawa lina uwezo wa kuvuna maji ya mvua ya ujazo wa mita 849,890.63 (849,890.63 m3) zenye uwezo wa kumwagilia jumla ya hekta 211 sawa na ekari 527.5  za mpunga. Eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika eneo hili ni hekta 554 (1,385 ekari).Mradi kwa sasa unaendeleza hekta 122 (ekari 305).

Msimu wa 2012/2013 kuanzia tarehe 01.12.2012, kampuni ya Geocon Company limited ya Box 6354 Dar es Salaam ilianza kujenga baadhi ya miundo mbinu ya umwagiliaji kwa gharama ya shilingi 177,011,480.00 na kukamilisha 24.04.2013.

Mwaka wa fedha wa 2015/2016 tarehe 20.06.2016, Halmashauri ilipokea fedha za kuendeleza mradi wa Ussoke Mlimani jumla ya shilingi 331,000,000.00 kutoka mfuko wa SSIDP. Fedha zote zilihamishiwa kwenye akaunti ya walengwa ya Umoja wa Watumiaji maji ya Umwagiliaji Ussoke Mlimani/Yela Yela (UMWAMUUYE).Umoja huu una wanachama 239 kati yao wanawake 117 na wanaume 122.

2.1 UTEKELEZAJI MRADI KWA KUTUMIA FEDHA ZA SSIDP

Fedha za utekelezaji wa mradi zimeanza kutumika mwaka wa fedha 2016/2017 baada ya kukamilisha taratibu za zabuni za kumpata mkandarasi.Kampuni ya M & A Engineering ltd. and Manguto investment co. ltd. (JV)  ya S. L. P. 1182, Shinyanga imesaini mkataba namba LGA/122/2016 /2017/W/20 tarehe 25.10.2016 na kuanza kazi 03.11.2016. Kazi itakazotekelezwa kwenye mkataba ni za shilingi 321,870,627.24 ( Pamoja na VAT). Mkandarasi ameishakamilisha kazi zilizoainishwa kwenye mkataba.Jedwali Na.1 linaonyesha miundo mbinu iliyotekelezwa katika skimu.

Table 1: MIUNDO MBINU ILIYOKAMILIKA SKIMU YA USSOKE MLIMANI

SN
MIUNDOMBINU ILIYOPO
KIASI
KIZIO
MAELEZO
1
Mfereji mkuu uliojengwa kwa mawe (MC)
175
m

2
Mfereji mkuu wa kati Namba 1, uliojengwa kwa mawe (SC1)
1350
m
Meta 25 za mwisho zimechimba tu.

3
Mfereji mkuu wa kati Namba 2, uliojengwa kwa mawe (SC2)
878
m
Meta 47 za mwisho zimechimba tu.
4
Mifereji 3 ya mashambani (TCs) upande wa SC1
345
m

5
Mifereji 4 ya mashambani (TCs) upande wa SC2
742
m

6
Mitaro 2 ya pembeni (CD) pembeni mwa barabara ya SC1 na SC2
2115
m

7
Mitaro 2 ya pembeni (CD) karibu na bwawa
264
m

8
Barabara 2 za huduma (SR) pembeni mwa, SC1 na SC2
2035
m

9
Vigawa maji (DB) kwenye SC1 kila inapounganika na TC
11
No.

10
Vigawa maji (DB) kwenye TC1/SC1
2
 

11
Vigawa maji (DB) kwenye SC2 kila inapounganika na TC
9
No.

12
Daraja la mfereji (Flume), kwenye SC1
1
No.

13
Punguza kasi (Drop) kwenye SC1
2
No.

14
Punguza kasi (Drop) kwenye baadhi ya TCs
13
No.

15
Daraja mbonyeo (Drift) kwenye barabara pembeni mwa SC1
1
No.

16
Njia ya maji kwenye mfereji SC1 (Cross Drainage)
1
No.

17
Vivuko vya wanyamakazi
2
No.

18
Vivuko kwenye DB
14
No.

19
Mageti ya chuma DB ya SC1na SC2.
2
No.

20
Tupio la maji (Spillway)
1
No.

21
Bwawa na miundominu yake ya kufungulia maji
1
No.

 

Kibanio cha Maji Mtaro wa Kutilisha Maji Shambai Shamba linapokea Maji ya Mradi


3. MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA MRADI NA WAKULIMA

Kamati ya ujenzi wa mradi imejengewa uwezo wa kusimamia mradi kupitia mafunzo ya usimamizi wa ujenzi sambamba na mafuzo ya usalama wakati wa ujenzi ambayo yalitolewa na Halmashuri ya wilaya ya Urambo ikishirikiana na mradi wa TANCAID II. Pia wakulima wameshapata mafunzo ya kilimo bora cha mpunga kupitia shamba darasa lililolimwa msimu 2015/2016 na kuvuna gunia 27 kwa ekari ukilinganisha na mavuno ya wakulima kwenye ekari ni gunia 10-15. Mradi una lengo la kuboresha uzalishaji wa mpunga kutoka uzalishaji wa tani 02 kwa hekta hadi tani 06. Wakulima 50 wameshiriki kulima mashamba yao msimu 2015/2016.Msimu huu 2016/2017 wakulima wa skimu wameuziwa mbolea ya ruzuku aina ya Urea jumla ya mifuko 60 ili kuboresha kilimo chao cha mpunga.

4. CHANGAMOTO NA UTATUZI WAKE

Changamoto iliyojitokeza ni mvua zilizokuwa zinanyesha zilipunguza kasi ya ujenzi.Mkandarasi aliomba kuongezewa muda na akakubaliwa kwa kuongezewa muda wa siku 30 ambazo zitakamilika tarehe 01.05.2017.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MTENDAJI URAMBO ASHIRIKIANA NA MAAFISA KUCHANGIA VIFAA VYA WANAFUNZI WA UMITASHUMTA NA UMISSETA

    May 13, 2025
  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.