• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Urambo  District  Council
Urambo  District  Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Urambo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu msingi
      • Elimu sekondari
      • Idara ya Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Fedha
    • Kata
      • Kata Zetu
    • Kibali cha Safari
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kiutumishi
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
      • Mwaka 2020-2025
      • Mwaka 2015-2020
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Afya, Elimu na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati Nyinginezo
        • Kamati ya Ugawaji wa Viwanja
        • Kamati ya Ajira
        • Kamati ya ALAT Mkoa
        • Wajumbe wa Mamlaka ya Mji Mdogo
    • Ratiba ya Vikao
    • Taarifa mbalimbali
  • Miradi
    • Miradi Mipya Itayotekelezwa
    • Miradi inayaoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Sheria
    • Taarifa
    • Taratibu
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Matukio
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video

Mwarobaini wa Makanpuni ya Simu Janja Janja Wakaribia

Siku iliyowekwa: March 17th, 2021

Na Edward C Rumanyika-Urambo DC

Naibu waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Andrea Mathew (MB) akiwa ameambatana na wataalamu kutoka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na viongozi wa  makampuni ya Mawasiinao ya simu ya Airtel, Halotel, TiGo, TTCL na Vodacom, amefanya ziara ya kutembelea maeneo yenye changamoto za mawasiliano ya simu na redio katika wilaya ya Urambo.  

Ziara hiyo iliyofanyika 16 Machi, 2021 Mhandisi Kundo Andrea Mathew aliweza kufanya mkutano wa ndani katika ukumbi wa mkuu wa wilaya ya Urambo na kisha kutembelea maeneo yenye changamoto zaidi ya mawasiliano katika kata za Songambele kijiji cha Mlangale, Kasisi jijiji cha Wema na Uyumbu kijiji cha Nsogolo kwani Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ilitoa ruzuku ya kiasi cha Tsh 117,500,000 kufikisha huduma ya mawasiliano kata ya Kasisi vijiji vya Azimio,Kasisi, Mapambano na Wema ili kutatua changamato ya mawasiliano katika vijiji husika.

Mhe Naibu waziri ameweza kubaini kuwepo kwa janja janja ya baadhi ya makampuni ya simu za mkononi kwenda kinyume na mikataba yao  kwa kuchelewesha kuhuisha teknolojia ya  huduma ya awali ya mawasiliano (2G) na kwenda kwenye teknolojia ya kisasa  ya mawasiliano yenye kasi zaidi (3G/4G) ili kuwafikia wananchi wengi kwa huduma nzuri na bora, licha ya kupokea fedha kutoka  Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) za kujenga minara na kuboresha mawasiliano maeneo yasiyo na mvuto wa biashara kwa watoa huduma za mawasiliano wamekuwa wakienda kinyume na mkataba yao.

Kutokana na hali ya udanganyifu uliobanika wakati wa ziara hiyo, Mhe. Mathew ameeleza namna Serikali ya Awamu ya Tano kupitia TCRA imejipanga kuhakikisha inathibiti  makampuni ya simu kwa kupima ubora wa huduma ya sauti, ujumbe mfupi na kufikia 2 Aprili, 2021 kutakuwepo na programu ya rununu (mobile App) itakayoratibu matumizi ya vifurushi vya intaneti kupitia simu ya mteja na tayari faini na adhabu zimeanza kutolewa kwa baadhi ya makampuni na TCRA.

Akihutubia wananchi wa kijiji cha Nsogolo kata ya Uyumbu Mhe. Mathew alipongeza ushirikiano wa dhati  ulipo kati ya ofisi ya  Mkuu wa wilaya, Mbunge wa Jimbo la Urambo na Mkurugenzi Mtendaji katika swala zima la kuwaletea maendeleo wananchi wa Urambo na hakusita kusema hiyo ndiyo chachu ya yeye kuja kujionea hali halisi ya changamoto za mawasiliano wilayani Urambo hasa vijijini.

Aidha aliwapongeza wananchi waliojitokeza na kuelezea kero za changamoto ya  mawasiliano  ya simu wanayopitia na kuwaomba kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha mpito kwani Serikali ya Awamu ya Tano inafanyia kazi changamoto hizo na kueleza ya kuwa   "sasa hivi habari ya vifurushi kuisha muda wake na kupotea sahau maana tumeyataka makampuni yote ya simu kuhakikisha mteja anaweza kuhamisha kifurushi chake kwenda kwa mtu mwingine au ata kuhuisha kifurushi kwa kununua kifurushi kama cha awali na vifurushi vitaungana ili muendelee kufurahia huduma na tutasimia hili" alisisitiza Mhe. Naibu waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

 Akizungumza kwa  niaba ya wananchi wa Urambo, mkuu wa wilaya ya Urambo, Mhe. Angelina Kwingwa amempongeza Naibu waziri kwa ziara yake katika wilaya ya Urambo na hasa kwa maamuzi yake yenye tija ya kufika vijijini ambako changamoto ya mawasilino ni kubwa na kueleza faida ya ziara hiyo itasaidia wananchi wa Urambo na Taifa kwa ujumla  kwa sababu  baadhi ya makampuni ya mawasiliano ya simu yalikuwa yanadanganya kutoa huduma ya kisasa yaani 3G/4G kumbe hali bado ni 2G uko vjijini maana hapakuwepo na uthibiti.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi za vijana za kujiunga na JKT 2024/2025 October 02, 2024
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI May 01, 2025
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili September 21, 2024
  • Tangazo kuhusu urejeshwaji wa mikopo ya vikundi vya vijana, wanawake na walemavu October 02, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MHE. DKT. MKANACHI AZINDUA ZAHANATI YA KINHWA

    April 25, 2025
  • URAMBO YAADHIMISHA MUUNGANO KWA MATEMBEZI, USAFI NA KUPANDA MITI

    April 26, 2025
  • KAMATI YA FEDHA UONGOZI NA MIPANGO, YATEMBELEA KITUO CHA AFYA NA NYUMBA ZA WAKUU WA DIVISHENI

    April 25, 2025
  • URAMBO YAFANIKISHA KIKAO CHAKE CHA KWANZA KUPITIA E-BOARD

    April 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri wa maji, Prof. Makame Mbarawa
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep DOCUMENTATION
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • BEMIS
  • Wahe. Madiwani

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa
  • Tovuti ya sekretarieti ya Ajira
  • Fomu ya Maadili ya Viongozi kwa Mtandao
  • Public Service
  • Matokeo ya Mtihani wa Taifa Tanzania.
  • Ikulu

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Bomani Urambo

    Anunani ya posta: Mkurugenzi Mtendaji (W), 30 Br ya Boma Stendi, S.L.P 170. 45582 Urambo Tabora

    Simu ya mezani: +255 (0) 262 965 824

    Simu ya mkononi: DED GRACE:0786821141

    Barua pepe: ded@urambodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2025 Urambo . All rights reserved.